Mizizi ya Mbarika ‘Castor’ tiba ya Kisonono, Kaswende
Na
Komba Kakoa
KISONONO ama Gonorrhoea kama
unavyofahamika kwa lugha nyingine ni
ugonjwa unaoshambulia wanaume kwa wanawake ambao huambukizwa kwa njia ya
kufanya ngono zembe ‘bila kutumia kinga’.
Utafiti uliofanywa na Dk. CalvinMcDonald
kuhusiana na ugonjwa huu unabainisha kuwa kisonono upo kwenye kundi la Sexually
transmitted infection (STI) na unasababishwa na bakteria aitwaye Neisseria
gonorrhoeae au gonococcus ambaye hupenda kuzaliana kwenye maeneo ya joto, yenye
unyevunyevu yakiwemo maeneo ya shingo ya uzazi (cervix), nyumba ya uzazi
(uterus), mirija ya uzazi (fallopian tubes) kwa mwanamke na mrija wa kutolea
mkojo nje (urethra) kwa wanaume.
Bakteria hawa pia huweza kuzaliana
kwenye mdomo, sehemu ya haja kubwa mkundu na mara chache kwenye koo na
macho.Pia hupatikana kwa wingi katika shahawa na usaha unaotoka katika uume wa
mwanamme mgonjwa na katika majimaji ya ukeni.
Dk. McDonald anasema bakteria hawa
huambukizwa kutoka mtu mmoja hadi mwingine kwa njianyingi zikiwamo ngono zembe
kupitia uke, mdomo au sehemu ya haja kubwa au mwanamme anaweza kumwambukiza
gono mwanamke hata kama hakutoa shahawa (manii) wakati wa kufanya tendo la
ndoa, pia kuchangia vifaa vya kujistarehesha ambavyo havikuoshwa au kufunikwa
na kondomu, kama vibrators na vimwanasesere vya aina nyingine.
anasema mwanamke mwenye maambukizi ya
ugonjwa wa kisonono hupata maumivu makali wakati wa kufanya tendo la ndoa,
kupata homa kali, kutokwa na uchafu ukeni wenye rangi ya njano au kijani,
kuvimba eneo la uke, kutokwa damu katikati ya siku za mwezi, kutokwa damu baada
ya kufanya tendo la ndoa, kutapika.
Kadhalika hupata maumivu ya tumbo na
maumivu ya nyonga, pia maumivu makali wakati wa haja ndogo na kupata haja ndogo
mara nyingi, kutoa uchafu kwenye njia ya haja kubwa, kuwashwa, maumivu au kutoa
damu wakati wa haja kubwa. Kukauka koo, kuwashwa, kumeza kwa shida au uvimbe
kooni, maumivu kwenye macho, kutopenda mwanga mkali na au kutoa uchafu kwenye
macho unaofanana na usaha kuwa na joto kwenye maungio ya mifupa
MADHARA
YA KISONONO
anabainisha kuwa mama mjamzito mwenye
maambukizi anaweza kumwambukiza mtoto anayezaliwa na endapo mtoto huyo hatapewa
tiba, anaweza kupata upofu wa kudumu.
Anaongeza kuwa, mama mjamzito mwenye
maambukizi anatakiwa apewe tiba kabla ya kujifungua kwani bakteria wa kisonono
hawaambukizi kwa kubusiana, kushikana mikono, kuchangia bafu au taulo, mabwawa
ya kuogelea, vyoo, kuchangia vikombe na vyombo ya kulia kwa sababu wadudu hawa
wa kisonono hawana uwezo wa kuishi kwa muda mrefu nje ya mwili wa binadamu.
Kwa wanawake, kisonono ambayo
haikutibiwa inaweza kusababisha tatizo lijulikanalo kama Pelvic inflammatory
disease (PID) ambayo inaweza kuharibu
mirija ya uzazi na mara nyingine kusababisha ugumba.
Pia kisonono ambayo haikutibiwa inaweza
pia kusababisha mimba kutungwa nje ya nyumba ya uzazi (ectopic pregnancy), hali
ambayo inaweza kumhatarishia mwanamke maisha yake.
Kadhalika ugonjwa huu unaweza kumsababishia
mwanamke kuzaa njiti (mtoto kuzaliwa kabla ya siku) au mimba kuharibika ana pia
mwenye kisonono anaweza kumwambukiza kichanga aliye tumboni wakati wa uzazi na
kukisababishia kichanga upofu wa kudumu, maambukizi kwenye maungio ya mifupa au
maambukizi kwenye damu.
Kisonono huweza kusambaa hadi kwenye
mifupa na damu hali ambayo ni hatari kwa maisha. Mtu mwenye gono anaweza
kuambukizwa UKIMWI kwa urahisi zaidi.
Anasema kuwa ikiwa vipimo vimeonyesha
kuwa una kisonono, wewe na mwenzi wako wote mnatakiwa kutibiwa kwa kutumia
antibiotics na kuacha kujihusisha na masula ya mapenzi hadi hapo tiba
itakapokwisha. Baada ya kumaiza tiba, inashauriwa kujipa mapumziko ya angalau
miezi 3 kuhakikisha kuwa maabukizi yote yamekwisha.
TIBA
Kwa mujibu wa Dk. K. M. Nadkarni katika kitabu chake
kinachoitwa ‘Indian material medical’ toleo lwa kwanza ameandika kuwa mizizi
ya mnyonyo ina uwezo mkubwa wa kutibu magonjwa
mbalimbali yakiwamo kisonono na kaswende.
Mbali na magonjwa hayo Dk. Nadika
anayataja magonjwa mengine ya mafundo fundo, kwikwi, uvimbe, macho ya manjano,
kuumwa koo, kuwa yanatbika kwa kutumia
mizizi ya mme huu.
Jinsi
ya kutumia
Anasema unatakiwa kuchukua mizizi ya
mnyonyo kisha loweka kwa muda wa siku mbili kisha mtumiaji anywe nusu glasi
kila siku jioni kwa muda wa siku tatu kisha apumzike kwa muda wa wiki moja
aendee tena kama mwanzo.
Hakuna maoni