Ajali za boda boda zinavyogharimu nguvu ya Taifa
Mwendesha pikipiki akiwa amepakiza abiria zaidi ya mmoja (Mishkaki kama inavyoonekana pichani |
UKOSEFU
wa ajira na kutokuwapo vyuo vya ufundi
katika Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani, ni jambo linaliosababisha vijana wengi
kujihusisha na uendeshaji wa pikipiki.
Kutokana
na hali hiyo, vijana wengi wanaomaliza elimu yao ya msingi na sekondari hujikita
katika biashara ya hiyo inayofahamika sana kwa jina la Bodaboda.
Pia
inaelezwa kwamba ugumu wa maisha huchangia kwa kiasi kikubwa kwa vijana wenye
umri mdogo kujiingiza kwenyeb biashara hiyo bila kuwa na elimu ya usalama
barabarani licha ya kuwa ni hatari.
Hiyo
inatokana na vijana hao kujifunza kuchochoroni kwa kulipia kiasi cha shilingi
elfu mbili kwa siku ambapo mafunzo hayo huchukua siku mbili mpaka tatu.
Pia
imebainika kuwa vijana wengi wanaojishughulisha na kazi ya bodaboda ni wale
walioshindwa kuendelea na elimu ya sekondari kutokana na sababu mbalimbali hususan
changamoto za kimaisha.
Aidha
wapo ambao wanafanya kazi hiyo kutokana na msukumo kutoka kwenye vijiwe ambavyo
wamekuwa wakishinda kutwa nzima pamoja na rafiki zao wanaofanya kazi hiyo.
Juma
Bakari(17), mkazi wa kijiji cha Dundani, ambaye ni miongoni mwa vijana
wanaoendesha bodaboda anasema kuwa baada ya kumaliza elimu ya msingi mwaka
2015, hakufanikiwa kendelea na elimu ya sekondari, na kuamua kujiunga na kazi
hiyo.
Bakari,
anasema aliamua kujiingiza kwenye kazi hiyo baada ya kufundishwa na rafiki yake
aliyekuwa naye kijiweni na kumlipa kiasi cha shilingi 4,000/ kwa siku mbili.
"Nilifundishwa
na madereva wenzangu, siku mbili nikawa nimejua kuendesha vizuri, nikaanza kuomba
bodaboda ili niweze kuifanyia kazi kwa lengo la kupata fedha za kujikimu na
kusaidia wazazi wangu,''anasema.
pikipiki maarufu kama bodabpooda |
Abuu
Khalid (20), ni mkazi wa kijiji cha Mkamba
ambaye pia anajishughulisha na kuendesha bodaboda anasema chombo anachoendesha si
mali yake ila ameingia mkataba wa makubaliano na mmiliki.
Anasema
kuwa kujuana na rafiki ambao ni waendesha bodaboda ndio kumemfanya kujua
kuendesha kwa kuwalipa kiasi cha shilingi 5,000/ ambao pia walimsaidia kupata chombo
cha kuendesha.
Anaongeza
kuwa amekubaliana na mmiliki wa chombo hicho kumpelekea kiasi cha shilingi elfu
kumi, ambapo ameanza mwezi Januari mwaka huu ambapo ifikapo miezi 10, mkataba
utafika ukomo na kumpatia fursa ya kumiliki chombo hicho.
"Ninaendesha
bodaboda ya mtu kila siku napeleka shilingi elfu 10,000, ambapo kwa kipindi cha
miezi 10 nitakuwa nimekamilisha kiasi cha shilingi milioni tatu na
nitakabidhiwa usafiri huo ili uwe mali yangu,''anasema.
bodaboda ikiwa chini baada ya kupata ajali |
Kwa
upande wa Mwenyekiti wa kijiji Mkuranga, Dunia Said, anasema kuwa, makubaliano
yaliyopo kati ya dereva na mmiliki ni kupeleka pesa kila siku lakini hakuna
posho wala mishahara katika mikataba hiyo.
Nae,
Mkuu wa usalama barabarani wilayani, Mkuranga Hamidu Mtinginjora, anasema
ukosefu wa elimu ya usalama barabarani kwa madereva hao ndio chanzo cha kuwepo
kwa ajali za mara kwa mara.
Anasema
katika kipindi cha Machi hadi Mei mwaka huu, jumla ya ajali zilizotokea ni 10,
na kusababisha vifo 16, majeruhi 10.
Anaongeza
kuwa ajali hizo zimetokana na mishikaki, mwendo kasi na abiria kutovaa Helemet
(Kofia ya kujikinga).
"Madereva
wengi hawajui sheria za usalama barabarani, katika kubeba abiria zaidi ya
mmoja, mwendokasi, kutofunga mkanda, kutovaa Helemet, mtoto kubebwa katika
bodaboda au bajaji akiwa na umri chini ya miaka nane,''anasema.
Anasema
kuwa katika makosa hayo kila kosa faini inalipwa shilingi elfu 30,000, lakini
na wao wanatoza faini katika uvaaji wa kandambili kwa mwendesha bodaboda ambayo
inakuwa shilingi elfu 30,000.
Anasema
kuwa licha ya kuwatoza faini za mara kwa mara lakini bado tatizo ni kubwa kwani
hakuna mabadiliko ambapo ajali zinaendelea kutokea na kusababisha vifo na ulemavu wa kudumu.
Mtinginjora,
anasema kuwa sheria inapaswa kufanyiwa marekebisho na kuongeza adhabu ziwe
kubwa zitasaidia madereva kuwa makini jambo ambalo litapunguza ajali hizo.
Kwa
mujibu wa Mkuu wa Kitengo cha Elimu ya
Usalama barabarani Makao makuu ya Trafiki Dar es Salaam, Abel Swai anasema kipindi
cha mwaka 2008 ajali nchini zilikuwa 2,036, vifo 309na majeruhi 1931.
Mwaka
2009 ajali zilikuwa 3406, vifo 508 na majeruhi 3,475 ambapo mwaka 2013,
zilikuwa 6831, vifo 1,098 na majeruhi 6375.
Kadhalika
mwaka 2014 zilikuwa 4169, majeruhi 3884, vifo 928 ikiwa mwaka 2015 ajali
zilikuwa 2682,vifo 934 na kujeruhi 2370.
Pia
kuanzia Januari 2016 hadi Machi mwaka huu ajali zilikuwa 663 na kujeruhi 200,
ambapo vifo zilikuwa 559.
Kwa
upande wa Afisa habari wa Kitengo cha Mifupa (MOI) Almas Jumaa, anasema kuwa
kwa siku watu saba hufanyiwa upasuaji kutokana na bodaboda ambapo kati ya
majeruhi wanaopokelewa asilimia 60 hutokana na bodaboda.
Anasema
wahanga wa bodaboda ni vijana walio na miaka 18 hadi 40.
Aidha
Jumaa, anashauri kwamba ifikie wakati kuanzishwe mazungumzo kati ya watu wa
kampuni za bima za afya na hospitali ili kusaidia katika kutoa tiba kwa wagonjwa
hao kutokana na mzigo mkubwa kuachiwa MOI pekee huku kampuni hizo zikichukuwa
mamilioni ya fedha.
''Ajali
zinapotokea asilimia 60 hawana uwezo wa kujitibu, hutibiwa kwa msamaha, lakini
kampuni za bima zinanufaika pale ajali zinapotokea inatakiwa itengwe asilimia
ambayo inapelekwa katika hospitali kutoka katika kwenye kampuni hizo,''anasema.
Hakuna maoni