Ijue saratani ya damu (Leukemia) na tiba yake
Na Komba Kakoa
SARATANI ya damu au Leukemia kwa jina la kitaalamu, ni hali ambayo mwili unatengeneza seli nyingi sana nyeupe za damu, kuliko kiwango ambacho kinatakiwa mwilini, seli hizi hutengenezwa na uvimbe kitaalamu kama tumour ambao unakua ndani ya mifupa ya kutengeneza damu.
Tabibu wa Tiba Asili na mbadala
Othman Shem, kutoka Paseko Clinic iliyoko Tabata Relini jijini Dar es Salaam,
anasema kuna aina mbili za saratani ya damu ambazo ni acute na chronic.
Anasema acute ni aina ya saratani
damu ambayo seli nyingi nyeupe za damu ambazo hazijakomaa hutengenezwa ndani ya
mifupa (bone marrows), na kuongezeka kuwa nyingi sana hivyo huzuia mifupa
kutengeneza seli zingine za kawaida.
“Mara nyingi saratani ya aina hii
huwapata watoto wadogo, japokua wakubwa pia wanaweza kupata ambapo inatakiwa
watibiwe haraka ili kuepukana na vifo vinavyotokea ndani ya miezi tangu mtu
kushambuliwa na tatizo hilo,” anasema.
“Chronic leukemia ni aina ya pili
ya saratani ya damu ambayo hutokea pale mifupa (bone marrows) inapotengeneza
seli nyingi nyeupe ambazo zimekomaa.
Anaongeza kuwa aina hii huchukua
miezi au miaka kusambaa mwilini na matibabu yake hucheleweshwa mpaka mgonjwa
atakapoonekana anafaa kuanza matibabu.
Kwa mujibu wa Shirika la Afya
Duniani, jumla ya watu 24,500 wamefariki ambapo kati yao 14,300 ni wanaume na 10,200
ni wanawake mwaka 2017.
Mwaka 2009 hadi 2013, vifo
vilivyotokana na leukemia vilikuwa vingi kwa wanaume na pia vilishika namba
sita kwenye orodha vifo vilivyoua
wanawake zaidi ya saratani nyingine.
Aidha WHO linasema vipimo vya
saratani kwa mwaka huu vinaonesha kuwa asilimia 10.2 ya wagonjwa wapya 1,688,780 wanasumbuliwa na
saratani ya damu nchini Marekani.
Aidha kwa mwaka uliopita zaidi ya
watu 1,290,773 walibainika kuwa na saratani ya damu
Kipindi cha miaka mitano tangu
mwaka 1975 hadi 1977, kulikuwa na wagonjwa wa saratani ya damu kwa asilimia 34.2.
Na kuanzia mwaka 2006 hadi 2012, kulikuwa
na asilimia 62.7, ambapo asilimia 94.1 walikuwa watoto wenye umri chini ya
miaka mitano na asilimia 93 ya watoto wenye umri chini ya umri wa miaka 15.
CHANZO
Kwa upande wake Salehe Mgonza
kutoka Hospitali ya Kairuki jijini Dar es Salaam anasema kuna mambo ambayo
yanaweza kuchangia kuanza saratani ya damu ikiwa ni pamoja na kupigwa na mionzi
ya jua au x ray za hospitali ambayo kwa namna moja ama nyingine huharibu uwezo
wa mwili kuamua ni kiasi gani cha seli kitengenezwe kwa wakati gani.
“Pia dawa zinazofanya kazi kwenye
seli ambazo pia nyingine ni za kupambana na saratani zikiwamo methotrexate
husababisha tatizo hilo,”anaongeza Dk. Shem
Dk. Mgonza anasema mtu akivuta au
kugusa hewa ya kemikali ya benzene ambayo hutumika viwandani na kwenye sigara
na kiasi kidogo kwenye mafuta yanayotumika kwenye gari, mifuko ya plastiki,
gundi na rangi za kupaka mbao za viti na makabati anaweza kupata ugonjwa huo.
Aidha, kushambuliwa na baadhi ya
virusi wajulikanao kama htlv huweza kusababisha saratani ya damu.
“Hata mtu kama kinga ya mwili wake
umeishiwa kinga kuna uwezo wa kupata tatizo hilo kwani kinga ya mwili hupambana
na kumaliza matatizo na kasoro zinazojitokeza kwenye mwili na kumuweka mbali na
magonjwa,”.
Pia tatizo hilo hutokana na kurithi,
kwani baadhi ya koo zina vimelea ambavyo hurithishwa kutoka wazazi kwenda kwa watoto,
aina za saratani za kurthi ni mbaya sana kwani huweza kumaliza ukoo mzima.
“Matumizi ya kemikali za mbolea
na kuulia wadudu shambani kitaalamu kama organophosphate huweza kusababisha
tatizo hilo,”.
DALILI
Dk. Jason Yovandich, wa Shirika
la Frederick National Laboratory (FNLCR) lililoko chini ya Taasisi ya Utafiti
wa Tabia za Saratani nchini Marekani anasema dalili za acute leukemia ni kuishiwa
damu, homa, kutokwa na damu sehemu mbalimbali kama puani, mdomoni, choo kubwa, machoni
na matundu yote ya mwili, kupata maumivu kwenye mifupa na jointi za mwili, kuvimba
maini, kuvimba bandama, kuugua mara kwa mara.
“Mara nyingi seli za saratani
zikifika kichwani mgonjwa huanza kuumwa kichwa, kupata kizunguzungu,
kichefuchefu na kutapika,
Dk. Yovandich anasema kwa upande
wa chronic dalili zake ni kuchoka sana, kupungua uzito, kushindwa kupumua, maumivu
ya tumbo, kutokwa jasho usiku, homa na moyo kukimbia, kuvimba kwa tezi, maini
na bandama, kuishiwa damu, kinga ya mwili kushuka,” anaongeza.
TIBA
MBADALA
Dk. Shem anasema ili kupambana na
magonja ukiwamo saratani za aina mbalimbali mtu anatakiwa kutumia virutubisho
vyote muhimu.
Anaongeza kuwa mara nyingi matibabu
ya saratani yana madhara makubwa sana mwilini lakini mtu akitumia virutubisho
vyenye vitamini mbalimbali huweza kumsaidia mgonjwa kupata nafuu na kupona
haraka na kutopata madhara mengi.
“Virutubisho hivyo ni vile vyenye
mchanganyiko wa vitamin nyingi ambazo kwa kawaida huzuia saratani ambavyo ni vitamin
C, vitamin E, vitamin A na nyingine nyingi.
Virutubisho hivyo ni muhimu sana
kwa wagonjwa wa saratani kutokana na ukweli kwamba wanakuwa na uwezo mdogo wa
kula.
Matibabu ya saratani hii
hutegemea aina ya saratani, kusambaa kwa saratani., umri na matibabu ya awali
ambayo huhusisha dawa, mionzi, kuongezewa damu na kupandikiza.
Tiba hizi huwa ni kwa ajili ya
kupunguza dalili, kuua chembe hai zisizo kawaida na kuongeza kinga ya mwili.
Kula lishe yenye mboga za majani
na matunda itasaidia kukinga mwili na magonjwa na kuongeza damu, tumia mafuta
ya samaki yana omega-3 fatty acid ambayo huzuia uzalishaji wa chembe za damu zisizo kawaida kwa wingi na
kuruhusu zile za kawaida kwa ajili ya kulinda mwili.
“Pata chanjo za mara kwa mara ili
kuzuia maambukizi kwani saratani hii huvutia sana maambukizi kutokana na
kushusha kinga ya mwili, fanya mazoezi mepesi mara kwa mara,”.
Kunywa juisi glass moja kila
asubuhi itasaidia kuimarisha mwili na kuongeza kinga na uepukane na matumizi ya
pombe, sigara na tumbaku.
========
Nimekuelewa sana muelimishaji
JibuFutaNimekuelewa sana muelimishaji
JibuFutaNimeelewa ila nlitaka kujuaa inatbka na kuisha kbsa
JibuFuta