VIUNGO AU MWILI KUJAA MAJI ( EDEMA )
Na Komba Kakoa
EDEMA ni tatizo la viungo au mwili kujaa
maji na kuonekana kama uvimbe kutokana na magonjwa ya moyo ambayo husababisha ushindwe kufanya kazi zake
vizuri hali ambayo husababisha damu kushindwa kufika katika maeneo mengine
yakiwamo miguuni.
Hali hiyo husababisha mwili kukusanya na
kuhifandi maji mengi zaidi ya mahitaji halisi na matokeo yake baadhi ya sehemu
au mwili mzima hujaa na kuonekana kama umevimba.
Mbali na moyo kushindwa kufanya kazi
yake, lakini pia matatizo ya mzio ‘Allergic Reactions’ yanaweza kuwa chanzo cha
edema kwani kwa namna moja au nyingine inawezekana mwili umepatwa na chembe
chembe ambazo haziendani na muundo mzima wa mwili.
Mfano wa chembe chembe hizi zinaweza
kutokana na vyakula, mafuta ya kujipakaa au hata sumu baada ya kung’atwa na
mdudu ambavyo vyote kwa pamoja husababisha mwili ujae maji hayo na kuwa katika
muonekano wa uvimbe.
Christian Nordqvist ambaye ni mtaalamu
wa masuala ya mfumo mzima wa mwili mwaka 2003 kupitia jarida la ‘Medical News’
aliandika kuwa magonjwa ya ini ( liver cirrhosis ), ambayo hupunguza utendaji
kazi wa ini ikiwa ni pamoja na utengenezaji wa vitu muhimu vinavyopatikana
katika damu mfano protin (albumin) huweza kusababisha edema.
Anasema chanzo kingine ni pamoja na
upungufu wa protini mwilini ambao husababishwa na matatizo ya kuwa na lishe
duni au magonjwa ya ini, pamoja na magonjwa ya figo ambayo hupunguza
utengenezaji wa damu mwilini kutokana na kuathiriwa kwa vitu muhimu katika figo
vinavyohusika na damu ( erythropoietin ).
“Inawezekana mtu mwili wake ukajaa maji
kutokana na kuongezeka kwa mahitaji ya mwili, mfano ni wamama wajawazito ambao
baadhi yao huwa wanavimba miguu kutokana na miili yao kuwa na ongezeko la
mahitaji ya damu ili kuweza kuutoshereza mzunguko mzima hadi kufika kwa
kiumbe/viumbe walioko tumboni,”.
Mtaalamu huyo aliandika kuwa ngozi hujaa
maji au kuvimba baada ya uwezo wa mishipa ya damu kuruhusu maji kupita
‘permiability’, kubadilika ambapo
mishipa hiyo ya damu huruhusu maji mengi zaidi yapite au yahame kutoka katika
mchanganyiko wa damu na kuhamia katika tishu au nyama za mwili nje ya mishipa
ya damu.
“Kwakuwa maji hayo hayapo katika mishipa
ndio chanzo cha sehemu ya mwili kuonekana kama imevimba hali ambayo huruhusu
kinga za mwili au seli zinazohusika na ulinzi wa mwili zifike kwa wingi zaidi
katika sehemu hiyo na kupambana,”
Anasema mapambano hayo katika sehemu
hiyo ni kwa lengo la kuziwezesha seli hizo zirejee katika utendaji kazi wake wa
kawaida kutokana na maji hayo huwa na kiwango kikubwa cha seli zinazolinda
mwili ambazo ni seli hai nyeupe za damu zinazofahamika kitaalamu kama
leucocytes,”.
Anasema tiba ya tatizo hili hutofautiana
kutokana na chanzo cha hali hiyo, hivyo matibabu hutofautiana hivyo ikiwa mtu
atakumbwa na tatizo hili anatakiwa kufika katika kituo cha afya kilicho karibu
iuli aweze kupata huduma.
TIBA
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa mwaka
2002 na Taasisi ya Tafiti za Magonjwa na Tiba asili ijulikanayo kama ‘European
Histamine Research Society’, ulibainisha kuwa ili kutibu edema muathirika
anatakiwa kuchua sehemu iliyoathirika.
“Kuchua sehemu hiyo kwa kutumia mafuta
ya mzaituni ‘Olive Oil’ kutasaidia
uvimbe kupwaya na kushuka kabisa hivyo
mtu atapata nafuu na kupona kabisa.
Mbali na mafuta ya mzaituni lakini pia anaweza
kutumia mafuta ya nazi ili kusugua taratibu sehemu yenye uvimbe, na ikiwa
mwenye tatizo ni mjamzito massage ifanywe na mtaalamu wa tiba ‘Therapist’ ili
kuepuka matatizo yanayoweza kujitokeza.
Nimeioenda makala hii ahsante kwa chapisho lako
JibuFuta