Breaking News

Wapandishwa kizimbani kwa wizi



Na MWANDISHI WETU
WAKAZI  wa Kinondoni  Thadeo Paul (28), Julius John (32) wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Mwanzo Kinondoni jijijini Dar es Salaam kwa kosa la wizi.
Wakisomewa shtaka lao mbele ya Hakimu Ester Kihiyo, Polisi mwendesha mashtaka Mrisho Warioba, alidai kuwa mnamo Februari 17 mwaka huu huko maeneo ya Kinondoni B jijini Dar es Salaam walivunja Baa ya Donasian Mkusa na kuiba majiko matatu ya kupikia, makreti matatu  ya bia vyote vikiwa na thamani ya Sh 1,750,000.

Aidha, washtakiwa walikana kutenda kosa hilo,dhamana zao zipo wazi alisema Hakimu Kihiyo.
Alisema kuwa washtakiwa watatakiwa kuwa na wadhamini wawili na bondi ya Sh 2,000,000 kwa kila mmoja.
Hata hivyo, kesi yao itasomwa tena Machi 6 mwaka huu na wakishindwa kutimiza masharti ya dhamana watarudishwa rumande.
Wakati huo huo mkazi wa Mbagala Mathias Hashim (30) amepandishwa kizimbanikatika Mahakama ya Mwanzo Kinondoni jijini Dar es Salaam kwa kosa la wizi.
Akisomewa shtaka lake mbele ya Hakimu Felister Massawe,Polisi mwendesha mashtaka Mrisho Warioba alidai kuwa mnamo Februari 21 mwaka huu huko maeneo ya Mikocheni kwa Warioba Kinondoni jijijni Dar es Salaam mshtakiwa aliiba rola mbili za nyaya za umeme zenye thamani ya Sh 80,000 mali ya Jun Dang.
Hakimu Massawe alisema kutokana namshtakiwa  kukana kutenda kosa hilo dhamana yake ipo wazi, atatakiwa kuwa na mdhamini mmoja na bondi ya Sh 100,000.
Kesi yake itasomwa tena Machi 9 mwaka huu alisema Hakimu Massawe.

Hakuna maoni