Breaking News

Asasi zataja vikwazo vya mwanamke



ASASI za kiraia zaidi ya saba nchini zimekutana kujadili lengo namba tano la malengo ya Maendeleo Endelevu ya Milenia (SDGs) ambapo walitaja changamoto zinazomkwamisha wanawake kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya Taifa.
Vilitajwa vikwazo hivyo kuwa ni pamoja na Ukatili wa kijinsia, mimba za utotoni, watoto wa kike kuachishwa masomo kutokana na matatizo mbalimbali.
Akizungumza katika Warsha ya mafunzo iliyoandaliwa na Taasisi za isiyo ya kiserikali ya Young Women’s Christian Assoiation of Tanzania (YWCA), Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Sheria kutoka Wizara ya Afya…, Vickness Mayao, alisema Serikali inaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wanawake ili waweze kuchangia pato la taifa.
“Tanzania ni mwanachama wa Umoja wa Mataifa hivyo tumesaini mikataba mbalimbali ambayo tumekuwa tukiitelekeza ikiwamo suala la Usawa wa kijinsi chini ya lengo la tano la Maendeleo endelevu ya millennia.
“wizara itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kama Asasi za kiraia kuhakikisha kila mwanamke anashiriki kwenye maendeleo ya Taifa,” alisema Vickness.
Kwa upande wake  Katibu Mkuu wa YWCA nchini, Dk Grace Soko, alisema mila na desturi zimekuwa kikwazo kikubwa kwa wanawake kushiriki katika shuguli za kiuchumi hivyo kushindwa kuchangia kikamilifu kwenye pato la Taifa.
“mafunzo hayo yamelenga hasa katika malengo ya millennia hususan katika lengo la tano linalosisitiza usawa wa kijinsia  hivyo tunatarajia washiriki watajadili na kujua jinsi gani ujumbe wa lengo hili kwa watu wa pembezoni.
“Kama inavyojulikana mwanamke anakabiliwa na vikwazo vingi vinavyosababisha hasishiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa mfano unakuta kuna baadhi ya mila na desturi zinaruhusu ndoa za utotoni, ukeketeji nakadharika kwahiyo inahitajin utolewaji wa elimu wa kutosha ili kuwabadilisha mitazamo,” alisema Dk Grace.

Hakuna maoni