Breaking News

Nasha MC:Chipukizi anayetamani viatu vya Diamond, P Square


Na Komba Kakoa
KWA wapenzi wa muziki wa kizazi kipya jina la Nasha MC si geni kutokana na kazi zake anazofanya ambazo huwapa burudani pindi wanaposikiliza.
Jina lake halisi no Juto Juma ambaye alizaliwa  mwaka 1989 huko Mkoani Morogoro katika kijiji cha Kichangani Tarafa ya Ngerengere, kata ya Tununguo.
Juto Juma 'Nasha MC'
Nasha anasema maisha yake hayakuwa na furaha kwani akiwa na miaka miwili wazazi wake walifarakana ambapo baba yake alitelekeza familia na kukimbia kusikojulikana.
“Baada ya baba kutukimbia, ndugu zake walianza kumnyanyasa mama na kufikia hatua ya kutunyang’anya mali lakini baada ya miaka kadhaa niliandikishwa kuanza masomo ya msingi katika shule ya msingi Tununguo,”
Anasema alisoma kwa shida sana kwani hakuwa na usimamizi wa wazazi wote wawili huku ndugu wa baba yake wakimkatalia kusoma ambapo baada ya miaka saba baadae baba yake alirejea nyumbani.
 HISTORIA YA MUZIKI
“Nilikuwa napenda sana muziki kwani nikiwa mdogo nilikuwa natengeneza viberiti kama maiki halafu naimba na kucheza ambapo majirani walikuwa wanafurahi,”.
“Pia baba yangu alikuwa msanii wa nyimbo za asili lakini hakuweza kunisaidia kukuza kipaji change kutokana na halihalizi za wazazi wa kiafrika kudharau vipaji vya watoto wao,”.
Majirani wengine walinipongeza huku baadhi yao wakisema nilikosa kazi za kufanya, lakini nilipokuwa ndio nikaona nifanye kweli kutumia kipaji changu
Nasha Mc

WIMBO WAKE WA KWANZA
Kwa mara ya kwanza kuingia studio ilikuwa mwaka 2011 ambapo nilirekodi wimbo uliofahamika kwa jina la  ‘Iweje sasa’ ambao ulihusu maisha yangu binafsi kulingana na halihalisi ilivyokuwa.
Anasema wimbo huo ulifanya vizuri  kwenye vyombo vya habari hususan katika kipindi cha ‘Hawavumi lakini wapo kinachorushwa hewani na kituo cha ITV na kufanikiwa kupata mtu ambaye alijitolea kumsaidia.
“Baada ya wimbo wangu kufanya vizuri kupitia ITV kuna jamaa alijitolea kunisaidia kutengeneza video lakini ghafla tukiwa katika matayarisho ya kushuti alipata safari ya kimasomo nchini Marekani na ikawa mwisho wa mipango yote ya kushuti tena,” anasema Nasha MC.
Aidha anasema baada ya wimbo huo alifanikiwa kurekodi wimbo mwingine unaoitwa  ‘Sijui kitu gani’ ambayo pia ilifanya vyema, ikafuatiwa na ‘ Damu yangu’ ambayo nilishirikiana na ‘Milo B’.
Anasema mwaka 2013 kaka yake aliyekuwa msaada mkubwa katika maisha na kazi zake alifariki jambo ambalo lilimrudisha nyuma na kushindwa kuendelea kwani hakuwa na mtu wa kumshika mkono.
“Kifo cha kaka yangu kilinipa mtihani mkubwa kwani siku na mtu mwingine wa kunisaidia kwakuwa yeye alikuwa kila kitu kwangu, hivyo nilishindwa kuendelea kufanya muziki na kujikutav mtaani nikihangaika jinsi ya kusimama tena.
Anasema katika kipindi hicho alijulikana kama ‘JT’ lakini baada ya kipindi cha mwaka mmoja na miezi mitatu kupita aliweza kusimama tena huku akijipa jina la Nasha MC na kuingia studio kutengeneza ngoma mpya.
Akiwa kama Nasha MC aliachia wimbo uitwao Enjo ambao upo tu hajausamba, huku akitengeneza ngoma nyingine mchanganyiko yenye mahadhi ya Mchiriku inayofahamika kama ‘Usiniache’ ambayo alimshirikisha Chid Benz.
Baada ya Usiniache ‘yaliyopo yapo’ ilifuata ambayo alimshirikisha PNC ambapo mpaka sasa amefanikiwa kufanya Kolabo na msanii wa Afrika Kusini anayefahamika kama Wajuze.
“Mashabiki wangu wakae mkao wa kula ‘Inuka ni ngoma kali ambayo imejumuisha sauti mbili kali yaani Nasha MC na Wajuze kutoka Afrika Kusini  ambayo ina mahadhi ya Mdundiko ni balaa,” anaongeza.
Nasha Mc

ANAZUNGUMZIAJE SOKO
“Kwakweli soko halisumbui kwasababu Nasha MC  anajichanganya, hafanyi kwenye muziki wa aina moja, kwani anacheza na mzunguko wa muziki na kuwasoma mashabiki wanataka nini,” anasema Nasha MC.
Nasha anasema amebahatika kupata mashabiki wengi wanaokubali kazi zake na ambao wamempokea vizuri jambo ambalo anaona ni deni kwao kuwatimizia kiu yao ya burudani.
“Kwakweli nina mashabiki wengi ambao wananipa hamasa na moyo wa kujituma ili nitengeneze kazi bora ambazo zitakata kiu nya ya burudani, pia naahidi nitaongeza ubunifu ili wasichoke kazi zangu,”
Anasema ubunifu ndio njia pekee inayoweza kuteka soko tofauti na wasanii wengine wanaokurupuka bila kutumia ubunifu, “Unamuonma ‘Diamond’ nakwambia muziki wake unapendwa kwasababu anacheza na akili za mashabiki wake,”

MAFANIKIO
Anasema anashukuru Mungu kwa kumuweza kusimama tena baada ya ku[itia misukosuko lakini sasa ameweza kumudu kuingia studio kurekodi ngoma kali ambazo zinazidi kupaisha jina lake.

CHANGAMOTO
Anasema kwa upande wake changamoto kubwa ni ukosefu wa menejimenti, kwani hana mtu wa kusimamia kazi zake jambo ambalo linampa wakati mgumu wa kufanya mambo yote.
“Ujue ukiwa na menejimenti mnagawana majukumu, jambo ambalo linachangia msanii kutengeneza kazi nzuri kwa kubuni vitu na ladha tofauti zinazovutia watumiaji, lakini bila menejimenti kwakweli ni vigumu sana.
Kutokana na kukosa menejimenti, Nasha MC anasema kuwa anahitaji kama kuna mtu ambaye anaona anaweza kufanya kazi naye ajitokeze ili aweze kumsimamia majukumu yake na kukuza muziki wake.
Nasha MC

MALENGO
“Malengo yangu ni kuwa msanii mkubwa hapa Tanzania, Afrika na Dunia kwa ujumla kwakuwa nina uwezo mkubwa wa kutunga nyimbo, kuimba na kucheza,”
Anasema anatamani kupiga hatua na kufikia kiwango alichofikia msanii Naseeb Abdul ‘Diamond’ pia wakali wa Nigeria Paul na Peter wanaounda kundi la Psquare ambalo linafanya vyema katika anga la muziki.
Anaongeza kuwa promosheni ndio inainua muziki wa msanii hivyo anaamini yote yanawezekana kama akipata msimamizi na mdhamini atakayeshughulikia maswala yote ili yeye ajikite zaidi kuumiza kichwa kwa kutunga nyimbo nzuri.

WASANII ANAOWAKUBALI
Kwakweli kwenye muziki wa bongo fleva wapo wasanii wengi wanaofanya vizuri lakini wanaonivutia zaidi ni Diamond platnums, Duly Sikes ‘Misifa’, Dudubaya na Selemani Msindi ‘Afande Sele’.

WITO
Wasanii tujitahidi kuwa na umoja ili tuweze kuifikisha sanaa yetu katika sehemu sahihi lakini tukiendelea kuwa katika matabaka hatutaweza kusaidiana kurekebisha kasoro pamoja na kupambana na changamoto zinazoikabili tasnia yetu

============  

Hakuna maoni