Same wapinga hukumu ya Mahakama--Na Mwandishi Wetu, Same
WANANCHI
wa Kitongoji cha Mkanyeni, Ruvu Mferejini Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro,
wameandamana hadi Mahakama ya Ardhi wilayani hapo kupinga hukumu iliyotolewa na
mahakama hiyo kumpa ushindi mwekezaji aliyevamia eneo lao.
Wakizungumza
wilayani humo wiki iliyopita, wananchi hao walimuomba Waziri wa Ardhi, Nyumba
na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, kuingilia kati mgogoro huo auliodumu
kwa miaka miwili ili kuepuka umwagaji damu unaoweza kutokea.
Alisema
baba na mama yake walizaliwa katika ardhi hiyo yenye miundombinu bora kwa
wakulima na wafugaji tangu mwaka 1958 lakini katika hali ya kushangaza, mwaka
jana alijitokeza mtu na kudai kuwa eneo hilo ni mali yake.
“Mtu
huyu anayejiita mwekezaji wala hana nyaraka zozote zinazoonyesha kuwa eneo hilo
ni mali yake,” alisema Songoi.
Alidai
kuwa hakuna kikao chochote cha kijiji kilichopitisha muhtasari wa kumkabidhi
mwekezaji huyo aliyejulikana kwa jina la IBIS International, lakini katika hali
ya kushangaza mwekezaji amewashitaki wananchi Baraza la Ardhi kwa mada ya
kuvamia eneo lake.
Bibi
kizee mwenye umri wa miaka 100 ambaye naye alishiriki maandamano hayo, Maria
Abrahamu, alisema yeye alizaliwa katika ardhi hiyo na wazazi wake ambao
wameshatangulia mbele ya haki.
Kikongwe
huyo alisema kwa sasa hajui hatima ya maisha yake baada ya mahakama kumpa
ushindi mwekezaji huyo kutokana na makazi yake kuwa ndani ya ardhi hiyo.
“Naiomba
sana serikali kutusaidia kutupa haki yetu kwa sababu hutujui ni wapi kwa kwenda
kuishi kwa sasa tumekuwa tukija hapa mahakamani kila kunapokucha lakini kilio
chetu hakisikilizwi,” alisema Bibi Maria.
Mwananchi
mwingine, Grace Mshana, alisema mwekezaji huyo amekuwa akiwanyanya na
kuwatishia maisha kwa silaha za moto, akidai kuwa hakuna mtu wa kumwajibisha.
Alisema
miaka yote wamekuwa wakifanya shughuli mbalimbali katika eneo hilo lakini
katika hali ya kushangaza, mwaka jana akaibuka mwekezaji huyo na kudai kuwa
eneo hilo ni mali yake na kuanza kuharibu miundombinu ya umwagiliaji katika
mashamba ya eneo hilo.
Karani
wa Mahakama hiyo aliyekataa kutaja jina lake, aliliambia gazeti hili kuwa
anachokifahamu ni kuwa kesi hiyo imehukumiwa na aliyeshinda ni mwekezaji.
Chanzo:Raia Tanzania
Chanzo:Raia Tanzania
Hakuna maoni