Wanafunzi afya waitupia lawama wizara
WIZARA
ya Afya na Ustawi wa Jamii imejikuta lawamani ikidaiwa kuwanyima namba
wanafunzi wa vyuo mbalimbali vya afya wanaofanya wanaofanya mitihani ya mwisho
na wanaoendelea.
Wakizungumza
jijini Dar es Salaam wiki iliyopita, wawakilishi wa vyuo kadhaa walisema wazazi
na wanavyuo wamekuwa wakilalamikia hatua hiyo.
“Hatua
hii imechukuliwa na Kitengo cha Mafunzo Wizara ya Afya kwa madai kwamba
wanafunzi wamechelewa kulipia mitihani hiyo,” alisema mmoja wa wawakilishi hao
akiomba kutotajwa jina gazetini.
Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi stadi, Joyce Ndalichako |
Wawakilishi
hao walitoka katika vyuo vya St. Aggrey Mbeya, Musoma COTC, Sengerema,
Tandabuhi cha Mwanza, Royal Pharmacy na Chuo cha KAM cha Dar es Salaam.
Wote
walikiri kuwa vyuo vinatambua kuwapo kwa tarehe ya mwisho ya kupeleka majina ya
waliolipia mitihani.
“Kwa
hali ilivyo si Watanzania wote wenye uwezo wa kulipa ada hiyo miezi minne kabla
ya wakati; huwa ni ngumu sana. Wizara ilitaka malipo yakamilishwe Aprili, miezi
minne kabla ya mitihani yenyewe,” alisema mmoja wao na kuongeza:
"Mfano
wa usumbufu tunaoupata ni wanafunzi wa Chuo cha Tandabuhi waliosafiri hadi
kwenye vituo vya mitihani mikoa mbalimbali walikopangiwa na wizara lakini
wakakuta hawana namba. Huu ni usumbufu mkubwa.
Wawakilishi
hao walishangaa wizara kushindwa kutoa muda mrefu kwa wanafunzi kufanya malipo
wakati vyuo vingi hufanya hivyo.
Imefahamika
kuwa wanafunzi wengi walilipia mitihani yao kati ya miezi miwili na mitatu
kabla, lakini wizara imekataa kuwapa namba wakidaiwa kuchelewa.
“Tunaomba
serikali itambue kwamba Watanzania wa kawaida kipato chao ni cha shida. Unakuta
mzazi ana watoto zaidi ya wawili, wote wanasoma.
“Mgogoro
wa vyuo na Kitengo cha Mafunzo Wizara ya Afya ni wa muda mrefu. Vikao
mbalimbali vimekaa chini ya NACTE, mawaziri na uongozi lakini hakuna suluhu,”
alisema mdau mwingine.
Wadau
hao walimtaja Naibu Mkurugenzi wa kitengo hicho, Dk. Bumi Mwanasege, kama
kikwazo kwa wamiliki wa vyuo.
Chanzo: Raia Tanzania
Hakuna maoni