Breaking News

Mkulima amka sasa tumia fursa mtandaoni




Na Komba Kakoa
HAKUNA ubishi kwamba mitandao ya kijamii ni njia pekee inayoweza kurahisisha utoaji taarifa haraka kuliko njia zozote zile duniani.
Hii ni kutokana na maendeleo ya Sayansi na teknolojia ambayo inazidi kukua siku hadi siku jambo ambalo linaifanya dunia kuzidi kuwa kama kijiji.
Mkulima
Kutokana na hali hiyo mitandao ya kijamiin nayo inazidi kujipatia umaarufu kutokana na idadi kubwa ya watumiaji kuingia humo na kufaidi bidhaa hizo.
Mitandao hiyo ambayo husaidiwa na uwepo wa Intaneti nipamoja na WhatsApp, Tweeter, Istagram, Facebook, imo, SnapChart na mingine mingi.
Kutokana na umuhimu wake watu hukesha humo wakiperuzi kuona mambo mapya yanayojiri ulimwenguni na kujisomea mambo mengi kwa dhima ya kujipatia utaalamu kwayo.
Hii ina maana kwamba mitandao hiyo imekuwa ikiwezesha jamii kutambua mambo mbalimbali yanayoendelea ulimwenguni.
Kutokana na hali hiyo ni dhahiri kwamba wakulima ambao wamekuwa wakilalamika ukosefu wa utaalamu juu ya uchaguzi wa mbegu bora, jinsi ya kuandaa mashamba, misimu bora ya kupanda na ukanda unaostawi aina za mazao Fulani.
Kadhalika mitandao hiyo itaweza kuwasaidia kukutana na wataalamu wa maswala ya kilimo na kuwahojin maswala mtambuka juu ya kilimo husika ili wawee kujikwamua na changamoto mbalimbali.
Aidha kupitia mitandao hiyo, wakulima hupata fursa ya kuonyesha mazao na kuyatangaza kwa ajili ya kupata wateja, soko ambalo ni rahisi kuliko masoko mengine.
Kulingana na faida zake ni wazi kwamba mkulima unaweza kuonyesha mazao yakon katika hatua zote kuanzia upandaji na yakikaribia kukomaa wateja wataweza kuona na kuweza kufika tayari kwa manunuzi.
Ili uweze kujikwamua na kupiga hatua katika kilimo chako, mkulima unapaswa kutumia mitandao ya kijamii vizuri kwa kufanya maonyesho ya mazao yako kuliko kukaa na kusubiri mazao yakomae ndio uanze kuhangaika kutafuta soko.
===================== 

Hakuna maoni