Wazazi waweza kujengea watoto misingi ya afya
Na Mwandishi Wetu
KUHAMASISHA watoto wako
kula vyakula sahihi, kufanya mazoezi na kupunguza muda wa kuangalia televisheni
kunaweza kusitoshe kuwajengea tabia za kuimarisha afya. Pia unahitajika
kuongoza kwa mfano, watafiti wanashauri.
"Ingawa mchango
wowote ambao wazazi wanaweza kutoa ni mzuri, tumegundua watoto wana nafasi
kubwa zaidi ya kushika miongozo kama wazazi watakuwa wanatenda wanayoasa,"
anasema mwandishi wa utafiti huo, Dk. Heather Manson.
Hilo linamaanisha
kuwachukua wanao na kwenda nao uwanjani kucheza, kuweka vyakula salama kiafya
vipatikane kwa urahisi na kudhibiti muda wa kukaa kwenye televisheni, anasema
Manson, mkuu wa kitengo cha uhamasishaji afya, magonjwa sugu na udhibiti wa
majeraha katika Shule Kuu ya Afya ya Ontario nchini Canada.
Katika nchi za Marekani
na Canada, mtoto mmoja kati ya watatu ni menye uzito kupitiliza au mnene kupita
kiasi, hivyo kuwa katika hatari ya kupata matatizo makubwa ya kiafya. Madaktari
sasa wanajua kuwa kuishi kiafya kunajumuisha si tu kutembea zaidi, bali kukaa
muda mfupi zaidi -- kujihusisha na masuala machache yanayofanya mtu akae mahali
pamoja kama kuangalia TV au kuingia mtandaoni, watafiti wansema.
Kwa ajili ya utafiti
huu mpya, watafiti waliwapigia simu zaidi ya wazazi 3,200 wenye angalau mtoto
mmoja mwenye umri wa chini ya miaka 18 kwenye jimbo la Ontario. Wazazi
waliulizwa juu ya tabia zao kuhusiana na muongozo wa kitaifa wa mazoezi ya
mwili, milo yenye afya na muda muafaka kuangalia TV.
Nchini Canada, watoto
wenye umri kati ya miaka 5 mpaka 17 wanashauriwa kufanya mazoezi ya kutoka
jasho kwa angalau dakika 60 kwa siku. Kutegemeana na umri na jinsia, kanuni
zinashauri kula milo minne mpaka 8 ya matunda na mbogamboga kwa siku. Kuhusu
muda wa burudani ya kutazama TV, si zaidi ya saa mbili ndiyo mapendekezo.
Watafiti waligundua
kuwa wazazi ambao huwapeleka watoto wao katika maeneo ambayo wanaweza
kujishughulisha kimwili, kama viwanja vya kuchezea na kwenye programu za
michezo, walikuwa na mara mbili ya uwezekano wa kuripoti kuwa watoto wao
wametimiza matakwa ya muongozo wa michezo kuliko wale ambao hawakupeleka.
Wazazi ambao
walishiriki katika michezo hiyo na watoto wao walikuwa na asilimia 35 zaidi ya
uwezekano wa kuripoti kuwa watoto wao walifikia malengo, kulinganisha na wale
waliokaa nje ya viwanja.
Aidha, wazazi ambao
waliwezesha watoto wao kula matunda na mbogamboga katikati ya milo mikuu mitatu
ya siku walikuwa na uwezekano mara tano zaidi wa kuripoti kuwa watot wao
wametimiza matakwa ya muongozi wa lishe, utafiti uligundua.
Msisitizo katika mlo wa
pamoja kama familia na kupunguza kutazama TV kulisaidia, pia.
Wazazi ambao walikuwa
nyumbani lakini mbali na TV walikuwa na uwezekano wa asilimia 67 zaidi kusema
watoto wao walikula matunda na mbogamboga za kutosha. Na wazazi ambao waliweka
masharti katika kuangalia TV, 'tablets' na vifaa vingine vya kielektroniki
walikuwa na nafasi mara mbili zaidi ya kuripoti watoto wao walifuata kanuni za
kupunguza matumizi ya kuangalia vitu hivyo kwa siku.
"Mambo yote haya
yanahitaji jitihada za mzazi," Manson anasema, na anaeleza zaidi kuwa
matokeo yake yanalipa ugumu unaoweza kuonekana.
Matokeo ya utafiti huo
yanaendana na ambacho Stephanie Quirantes, mtaalamu wa lishe wa jumuiya,
aligundua katika programu zake kwenye Hospitali ya Watoto ya Nicklaus jijini
Miami. Moja inaandikisha vijana matipwatipwa na mama zao. "Tunataka kina
mama hao wajifunze juu ya mazoezi ya mwili na lishe," Quirantes alisema.
Kuongoza kwa mfano
kunalipa, alisisitiza.
"Haitoshi kusema,
'Fanya hivi,'" Quirantes anasema. Wakati vijana wanapoona mama zao
wanafuata tabia njema kiafya, inawahamasisha wao, pia. Matokeo yanaonyrsha
"tunaelekea kwenye uelekeo sahihi kwa ambacho tunafanya," Quirantes
anasema.
Kuwa na karoti na
matunda kwenye jokofu nyumbani kunasaidia.
"Kuwa na vitafunwa
hivi tayari tayari," alisema, ili watoto waweze kuchukua tu wakati
wakienda mazoezini michezoni au kucheza baada ya muda wa masomo. "Watoto
hawatomenya wenyewe matunda," anasema.
Quirantes anasema faida
zake ni kwa pande zote mbili. Kina mama wanaoshiriki na mabinti zao mara nyingi
huboresha tabia zao wenyewe kiafya, amegundua.
Makala hii ni kwa
mujibu wea jarida la HEALTHDAY
Hakuna maoni